Wanafunzi
Shule ya Msingi Luvulunge iliyopo kata ya Isapulano Wilayani Makete
Mkoani Njombe wameanza kunufaika na Elimu ya wasaidizi wa Kisheria
inayotolewa na Shirika la Makete Paralegal Organisation(MAPAO)
Mandhari
ya Shule ya Msingi Luvulunge iliyopo kijijini hapo kata ya Isapulano
Wilayani Makete yenye wanafunzi 134 kuanzia Darasa la kwanza mpaka
Darasa la sita
Mkurugenzi
wa Shirika hilo la Wasaidizi wa Kisheria Wilaya ya Makete DENIS SINENE
amesema utoaji wa Elimu hiyo kwa Wanafunzi ni katika kuwasaidia watoto
kuwa na Misingi bora ya Elimu na kujua haki zao za Msingi ikiwa ni
pamoja na wao kutambua wajibu wao
Mkurugenzi
wa Shirika hilo la Wasaidizi wa Kisheria Wilaya ya Makete DENIS SINENE
Ametoa Maelezo hayo wakati wa kuanzisha Klabu ya Wasaidizi wa Kisheria
Shuleni hapo ikiwa ni Mwendelezo wa kuanzisha Klabu hizo kwenye Shule za
Sekondari na Msingi Wilayani hapa
Akizungumza
na wanafunzi hao Denisi Sinene amesema “Tunafanya kazi za kuisaidia
jamii ya wanaMakete ikiwa ni pamoja na wazazi wenu,ndugu zetu ikiwa ni
pamoja na ninyi watoto mnapokuwa na Matatizo kwenye masuala madogomadogo
ya kisheria”
“Jukumu
letu tunaelekeza,tunashauri,tunapatanisha,tunaonya,tunatetea haki za
walemavu,tunafundisha sheria na haki za watoto,wazee na wanawake kwenye
kata zote ndio kazi tunazozifanya”Aliongeza Sinene
Mkurugenzi
huyo ameelezea dhamira na Lengo la kuwepo kwa Wasaidizi wa Kisheria
Wilayani hapa pamoja na kuwataka watoto kuwa watiifu kwa wazazi wao na
Jamii inayowazunguka
Denis
Sinene amesema “Dhamira ya MAPAO ni kuwa na Jamii inayotambua haki za
Binadamu na ninyi ni miongoni mwa Jamii,sasa tunataka jamii hii ijue
haki,kwa hiyo sasa Makusudi ya MAPAO inataka Jamii ijue haki na ninyi
pia mjue haki mbalimbali za Binadamu nanyi muwe na uelewa kuhusu haki
zenu”
Kwa
Upande wake Mjumbe wa Bodi ya MAPAO Ndg.Nahumu Tweve amesema wanafunzi
hao wakiendelea kupatiwa Elimu hiyo mara kwa mara Taifa litakuja kuwa na
Vijana waadilifu na kuyaishi mema wakati wote
Nahumu Tweve amesema
“Wapo wahalifu ndio maana ipo Sheria sasa ninyi mkilelewa katika
Misingi yenye Maadili naamini mtakuwa wazalendo,waadilifu,wenye unyoofu
na baadaye tutakuwa na Taifa lenye watu waelewa sasa ninyi shule ya
Msingi Luvulunge tunategemea mtakuwa mfano mzuri kwa watoto kutoka shule
zingine ndani na nje ya Wilaya ya Makete kwa kuwa na watoto
waadilifu,wanaojua sheria na wajibu wao”
“Tunategemea
hamtasumbua walimu,hamtasumbua wazazi,hamtalisumbua Taifa kwa sababu
mtakuwa mmeshaelewa wajibu wenu katika Jamii na hapa shuleni mtayaishi
yale tutakayokuwa tunawafundisha,na nyie mkawe mnawafundisha wengine
huko nyumbani”
Mkurugenzi
wa Shirika hilo la Wasaidizi wa Kisheria Wilaya ya Makete DENIS SINENE
amesema watoto wanatakiwa kujitambua kwa kujua wajibu wao kwa wazazi
huku Klabu ya wasaidizi wa Kisheria iliyoundwa hii leo shuleni hapo
ikiwa na wajumbe(Wanafunzi) Zaidi ya 40
Shirika
la Wasaidizi wa Kisheria Wilaya ya Makete MAPAO limeanzisha Klabu 2 za
Wasaidizi wa Kisheria kwa Wanafunzi,Klabu moja kutoka shule ya Sekondari
Iwawa kata ya Iwawa na Klabu nyingine imeanzishwa leo shule ya Msingi
Luvulunge iliyopo kata ya Isapulano na hii ni katika Mpango endelevu wa
kutoa Elimu ya Kisheria kwa wanafunzi shule zote za Msingi na Sekondari
Wilayani hapa
Picha mbalimbali kuhusu kilichofanyika leo Shuleni hapo Tazama hapa chini
Wanafunzi wa shule ya Msingi Luvulunge wakisiliza kwa Umakini Elimu iliyokuwa ikitolewa na Viongozi wa MAPAO
Kutoka
kulia ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Luvulunge Frolida Ilomo
akitambulisha wageni kutoka Shirika la MAPAO waliotembelea shuleni hapo
na kutoa Elimu ya wasaidizi wa Kisheria
Mkurugenzi wa Wasaidizi wa Kisheria Wilaya ya Makete Denis Sinene akizungumza na Wanafunzi wa Shule ya Msingi Luvulunge
Mkurugenzi
wa Wasaidizi wa Kisheria Wilaya ya Makete Denis Sinene akiimba wimbo wa
MAPAO pamoja na wanafunzi wa shule ya Msingi Luvulunge
Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa MAPAO Denis Sinene,katikati ni Mjumbe wa Bodi ya Mapao akizungumza na wanafunzi shuleni hapo
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi MAPAO Frolida Ilomo akizungumza jambo
Huu ni ubao wa Mahudhurio ya wanafunzi shule ya Msingi Luvulunge kwa wiki hii