Kutoka
kushoto ni Wananchi wa kata ya Tandala wakimuelekeza M/kiti wa Bodi ya
Mapao Wilaya ya Makete Ndg.Falmeo Mahenge(Kulia) wanavyosaidiwa mambo
mbalimbali yanayohusu usaidizi wa kisheria
Simon Henry kutoka Makao Makuu ya LSF Dar es salaam pamoja na viongozi mbalimba wa ufuatialiaji kutoka ngazi ya Mkoa wa Njombe akizungumza kuhusu Wasaidizi wa kisheria namna wanavyofanya kazi ya kuwasaidia wananchi katika kutatua migogoro na kupata haki akiwa ofisi ya Mkuu wa Wilaya Makete
Wageni hao walitembelea pia ofisi za Kitulofm Redio ambayo inafanya vipindi mbalimbali na wasaidizi wa Kisheria Wilayani hapa kila wiki mara moja
Timu
ya ufuatiliaji Ngazi ya Taifa kutoka Shirika la LSF Wasaidizi wa
Kisheria wametembelea na kuona Shughuli zinazofanywa na wasaidizi wa
kisheria ngazi ya Wilaya na kata Wilayani Makete Mkoani Njombe huku
ikipongeza kazi kubwa inayofanywa na wasaidizi hao na kuongeza kwamba
inafaa kuwa mfano wa Kuigwa na wasaidizi hao Wilaya zingine
Pongezi
hizo zimetolewa na Ndugu Joseph Shabani Magazi Afisa Mradi kutoka LSF
Zanzibar akiwa Wilayani hapa akiongozana na Simon Henry kutoka Makao
makuu ya LSF Dar es salaam pamoja na viongozi mbalimba wa ufuatialiaji
kutoka ngazi ya Mkoa wa Njombe
Vincent
Msigwa mkaazi wa kijiji cha Ikonda kata ya Tandala amesema uwepo wa
MAPAO umewafanya wananchi kujua mengi kuhusu migogoro na namna ya
kutatuliwa kwa kuwa yeye ni miongoni mwa waliosaidiwa na MAPAO
Akitolea
ushuhuda ameongeza kuwa alikuwa na mgogoro na jirani yake ambapo Mifugo
yake(Ng'ombe) ilikula mahindi ya jirani kilo tano na alishtakiwa kwa
Mtendaji wa kijiji na akaambiwa alipie Milioni mbili lakini baada ya
kukutana na Msaidizi wa kisheria kata ya Tandala Bw.Naumu Sanga na
kuwaeleza shida hiyo waliitatua kwa kulipa mahindi lita tano tu badala
ya fedha talimu Milioni mbili
Mkurugenzi
wa Wasaidizi wa Kisheria Wilayani Makete Mch.Denis Sinene amesema
Shirika la MAPAO kwa sasa limekuwa likifanya kazi kwa ufanisi mkubwa
kutokana na mafanikio wanayoyapata kwa kutatua changamoto na migogoro
mingi inayoikumba jamii hususani kwenye migogoro ya ndoa,Ardhi na
mirathi